DIAMOND KIBOKO, KAELEZA KILA KITU KUHUSU MOBETO

diamond achepuka na mobeto

Lile fumbo la muda mrefu kati ya Diamond na koo asiyeishiwa vituko Hamisa mwana wa Mobeto leo limefumbuliwa mchana kweupe! Sekeseke hilo lilianza wakati Hamisa akiwa mjamzito ambapo zilipatikana habari za chini kwa chini kuwa mimba hiyo ni ya mtu mzima Dangote.
Fukuto lilishamiri zaidi baada ya Hamisa kujifungua mtoto na kumpa jina la Abdul Nasib Abdul. Hapo watu wakakaa mkao wa kutamani kupata habari.

HATIMAYE JIBU LIMEPATIKANA

Akizungumza leo asubuhi Radio Clouds, Diamond alikubali kuzaa na Hamisa Mobeto ila akasikitishwa na jinsi koo huyo anavyotamba na kumfanya ‘maza hausi’ Zari ajisikie vibaya.
Alizidi kufafanua kuwa, yuko tayari kuhudumia malezi ya mtoto ambayo hata hivyo lazima yawe yanakubalika kisheria.

AOMBA MSAMAHA KWA KUCHEPUKA

Katika hali isiyotarajiwa, mkali wa Zilipendwa aliwaomba radhi mashabiki wake kwa kuwaangusha baada ya kuzidiwa na tamaa za mwili na kujikuta anachepuka na koo mwenye vurugu nyingi mjini.
Akiongea kwa msisimko alieleza kuwa anampenda sana mwandani wake, Zari na anajutia kwa yote yaliyotokea.

PICHA YA MTOTO

Picha ya mtoto tayari imesharushwa katika ukurasa wake wa Instagram na watu wanatoa maoni yao mbalimbali ikiwa ni mseto wa matusi na hekima za walimwengu.
Na: Daud Makoba

Shusha maoni yako kuhusu varangati hili…

POVU LA MWALIMU MAKOBA KWA WASANII WAVAA HOVYO

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne