MECHI YA CHELSEA NA BURNEY: MORATA AU BATSHUAYI?

MECHI YA CHELSEA NA BURNEY
Uwanja unaomilikiwa na timu ya Chelsea - Stamford Bridge.
VINARA Chelsea wanakwenda kufungua mbio za kuutetea ubingwa wao wa ‘Premier League’ kwa kunyukana na Burnley katika uwanja wenye hadhi ya juu – Stamford Bridge.

Baada ya kuipiga Arsenal mabao matatu kwa nunge katika mchezo wa kupasha misuli kabla ya ligi kuanza, na baadaye kupoteza michezo mitatu mfululizo dhidi ya: Bayern Munich, Inter Milan na The ‘Gunners’, kocha Antonio Conte hatazamii chochote ila ushindi.
Kwa upande wa timu ya pili, Victor Moses hatacheza kwa sababu ya kadi nyekundu aliyoipata katika fainali ya kombe la FA mwezi wa tano.
Swali linaloibuka ni nani ataziba pengo la winga wa kulia Moses? Ni lazima Conte atachagua kati ya Michy Batshuayi au mchezaji mpya Alvaro Morata.
Hata hivyo kutokana na aina ya uchezaji wa Morata, anapewa nafasi kubwa zaidi ya kuanza.
Toa maoni yako. We unafikiri nani ataanza?

IMEANDIKWA NA MOWASHA / NGEME


Shusha comment yako…

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Vichekesho vya Kuchekesha na Kuvunja Mbavu 1