Kwa Nini Una Kibamia? na Jinsi ya Kuepuka Madhara Yake

kwa nini una kibamia
NI tatizo linalosumbua vichwa vya wanaume wengi. Si wao tu, hata wanawake walioolewa na watu wa aina hii  hawaridhiki na hali, wanahisi kuna kitu wanakosa.
Kibamia, ama uume mdogo hupimwa kwa kuangalia ukubwa wa uume uliosimama. Uume wa kawaida huanzia sentimita 12. inaweza kuwa chini ya sentimita 12 na isiwe kibamia, kwa mfano, mwenye sentimita 11, 10 au 9, bado siyo kibamia. Hivyo basi, kibamia ni uume ambao hauvuki sentimita 6.
Kwa nini una kibamia? 😯
Sababu ya kwanza ni kurithi. Watoto wanapozaliwa hurithi vinasaba kutoka kwa baba na mama. Kama baba yako alikuwa na ‘kibamia’ basi hapana shaka yoyote hata wewe utakuwa hivyo.
Sababu  ya pili ni vyakula ulivyokula wakati wa ukuaji wako. Vyakula vyenye sukari na protini vinamsaada mkubwa katika ukuaji wa kiungo chako hicho nyeti. Kumbuka kwamba, huwezi kujenga ghorofa bila kuwa na matofali. Hivyo, vyakula ni nyenzo mojawapo inayosaidia kujenga maumbile.
Nifanye nini kuepukana na tatizo hili? ðŸ˜Œ
Kwanza natoa onyo. Usikimbilie kutumia madawa ya kuongeza urefu wa mashine yako. Mazoea haya yana madhara makubwa huko mbeleni ikiwemo kupelekea kansa au kupoteza nguvu za kiume. Njia sahihi ni kula vyakula vyenye virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini. Pia, kufanya mazoezi kuna faida kubwa. Hakikisha hupitishi siku bila kuuchangamsha mwili wako kwa mazoezi.
Kibamia kina madhara yoyote? 😡
Kwa kuwa kuwa na kibamia hakuna uhusiano wowote na upungufu wa nguvu za kiume, hakuna madhara yoyote kuwa na maumbile hayo. Kinachohitajika kwa mwanamke si ukubwa wa uume, bali ni msisimko unaosababishwa na uume uliosimama bila kujali ukubwa wake.
Hii ni kwa sababu, sehemu zinazohitaji msisimko kwa mwanamke zipo mwanzoni mwa uke wake.
Hata hivyo, kitendo cha kuwa na kibamia, kinaweza kukuathiri kisaikolojia kiasi cha kuona aibu hata pale unapokuwa na mwenzi wako kumuonesha kiwanda.
Nifanye nini zaidi? 😮
Jiamini na jikubali jinsi ulivyo. Kama nilivyosema awali, ukubwa wa uume haumaanishi kuwa na nguvu za kutosha kumridhisha mwenzi wako, wapo watu wana maumbile makubwa lakini hawana uwezo wa kumaliza hata nusu dakika. Hivyo, mwanaume mzuri ni yule anayemridhisha mpenzi wake bila kujali ukubwa wa ndonga!

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne