Kapalalai: Mc, Mchekeshaji, Mwanamuziki… Vipaji Lukuki!
Ni vigumu kuzungumzia tathnia ya vichekesho
bila kulitaja jina la Kapalalai kijana aliyetamba katika kipindi cha KANJANJA. Umahiri
wake wa kuigiza sauti ya kimasai ndio unaomfanya azikonge nyoyo za wamsikilizao
na kumtazama huku akiwaacha na kicheko kisichokuwa cha hiyari kwa jinsi
anavyoweza kupangilia vioja.
Katika muziki hajalaza damu. Mtindo wake wa
uimbaji naufananisha na ule wa marehemu Mr. Ebo. Hakika Kapalalai anatupunguzia
machungu ya kumpoteza mzee wa kamongo. Hata hivyo, katika aina yake ya uimbaji,
anaupekee wa kutosha unaomtofautisha na kumfanya awe yeye! Hiki ni kipaji
kikubwa walichonyimwa wengi. Kwa sasa, anatamba na wimbo wake uitwao BISHOO na
tayari amekwisha ufanyia video.
Miongoni mwa shughuli zinazotunisha pochi yake
ni ‘ushereheshaji’ (MC). Amepokea na anaendelea kupokea mialiko mingi ya
kusherehesha katika harusi nyingi na pengine si harusi pekee, bali shughuli
yoyote inayohitaji msema chochote, Kapalalai ataifanya vyema na hutajutia
kumuita. Unaweza kuwasiliana naye kwa simu namba: 0718 228 972.
Yapo mengi ya kumzungumzia Kapalalai, hayawezi
kuisha kwa siku moja, ila mengine unaweza kuyafahamu kutoka kwake kwa
kumfuatilia katika mitandao ya kijamii: facebook, ‘Mc Kapalalai’ na instagram, ‘mckapalalai’.
Wanamuita Kapalalai handsome ya boma, MZEE WA
CHEKA USIBOEKE!