Sarakasi za Makinikia: Wasomi Waliweka Elimu Mfukoni

Gari tatu zikipishana katika mgodi
Wasomi wengi katika nchi za kiafrika linapokuja suala la kusaini mikataba inayogusa rasilimali za taifa, huwekeza nguvu nyingi katika vidole huku vichwa vikiachwa vifanye kazi ya kubeba bongo tupu!
Inashangaza kusema kuwa, walioliingizia hasara taifa hili katika sakata la MAKINIKIA ni watanzania ambao kwa idadi yao hawazidi watano… wasomi, waliobeba bongo tupu, AKILI NDOGO ZINAZOENDESHWA NA TUMBO!
Makampuni ya wakala wa meli ya Freight Forwarders (T) Limited, Quick Services Clearing and Forwarding Limited na Walford Meadows Co. Ltd, ziliwasilisha nyaraka za uwongo za usafirishaji wa makinikia kutoka Kahama Mining Corporation, (baadaye Bulyanhulu Gold Mine Ltd) na Pangea Minerals Ltd, katika kipindi cha kati ya mwaka 1998 na 2017. Kwa miaka 19 wasomi wetu walikuwa wakidanganywa, nasi tukiwalipa kodi zetu watutumikie. UCHURO!
Katika maandiko yangu yaliyopita niliwahi kushauri kwamba, tusiwafundishe watoto wetu historia ya sayansi, bali tuwafundishe sayansi yenyewe! Ni ajabu wasomi wetu waliamini kwamba kilichokuwa kikisafirishwa ni mchanga mtupu, kana kwamba wazungu wale walikwenda kutengenezea matofali. Ukweli ni huu, mchanga uliouzwa nje ya nchi haukuwa mchanga hasa badala yake, yalikuwa ni madini ya aina mbali mbali mahususi yaliyopatikana kutokana na uchenjuaji kwa njia ya ‘carbon–inleach’ (CIL). MTANZANIA ALIYEFUNDISHWA HISTORIA YA SAYANSI BADALA YA SAYANSI HAWEZI AKAUJUA MFUMO HUU SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKE.
Madini mengi kama dhahabu, Silver, Copper, Sulphur, Iron, Nickel, Zinc na Madini yote ya  kundi la Platinum ambayo yalisafirishwa kwa kivuli cha mchanga, kama pesa yake ingekwenda  serikalini, serikali ingeweza kuajiri waalimu wote wa sanaa na sayansi na kuachana na porojo rojorojo kuwa waalimu wamejaa. Pia serikali ingeweza kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu hata wanaosoma mapishi wangepata 100%. Katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia, serikali ingeweza kuununua mtandao wa WhatsApp, facebook, twitter na instagram. AMINI MANENO YANGU, NAZUNGUMZIA DOLA ZA KIMAREKANI BILIONI 144.77 sawa na trilioni 380.499, pesa hiyo ikiandikwa kwa tarakimu asilimia 99 ya watanzania hawataweza kuisoma, 380,499,453,421,688.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne