UTAFITI; NCHI KUWA NA MATUKIO MENGI, CHANZO KINGINE CHA AJALI ZA BARABARANI KILICHOSAHAULIKA.
Anaandika Mtafiti; Daud
Makoba
Kuishi Tanzania ni kama
kuishi ndani ya luninga, matukio yanapishana kwa kasi ya ajabu, likitoka hili
laja lile basi vurugu mwanzo mwisho.
Ona mfululizo wa matukio
haya, MAUAJI, KESI, UTUMBUAJI, VIFO VYA VIONGOZI, TETEMEKO LA KAGERA, UHAKIKI
WA WATUMISHI, BUNGE LIVE, AJIRA, OPARESHENI UKUTA, FARU JOHN, KUTEKWA/KUJITEKA
KWA WASANII, VITA YA MADAWA YA KULEVYA, SAKATA LA DAUDI BASHITE, BOMOA BOMOA,
MVUA ZISIZOKATA, NJAA, UKAME, MKUU WA MKOA KUVAMIA KITUO CHA REDIO… yako mengi,
haiwezekani kuyataja yote.
Kivipi matukio haya
yanachangia kusababisha ajali za barabarani? Madereva wamegeuzwa wafuatiliaji
wa matukio haya ya kusisimua. Kila kukicha wanajiuliza leo litasemwa lipi na
kesho kitatokea nini? Katika kanuni za udereva, unatakiwa uweke akili yako yote
barabarani, hutakiwi kufanya chochote kile isipokuwa kuendesha gari lako. Kwa kuwa
udereva si sehemu ya kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja, kitendo cha madereva
hawa kufikiria zaidi matukio yanayotokea nchini, kinawafanya washindwe kuweka
akili yao katika safari. Kama hujatuliza akili yako katika gari unaloliendesha,
basi unaialika ajali.
Rai yangu ni kwamba;
wanasiasa waache kufanya mikasa, wafanye siasa. Kutamani kumulikwa na kamera za
waandishi wa habari kila wakati kunaliselelesha taifa letu katika kijito kidogo
chenye giza nene.
Mambo mengine
yanayosababisha ajali za barabarani ni, mwendokasi, ubovu wa barabara, ulevi na
rushwa za barabarani.