Mtihani wa Kiswahili Kidato cha Nne| Pre Necta| 28 Apr 18
Sehemu A Ufahamu (alama 10) 1. Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata: BAADA ya kusikia simulizi mbalimbali kuhusiana na ‘chuma ulete’ kwa muda mrefu, nikaamua nijaribu ili niweze kurahisisha maisha. Nilitamani sana zile hadithi za ‘chuma ulete’ ziwe kweli juu yangu. Ninunue bidhaa kisha fedha zinirudie, zikiwa nyingi zaidi. Nile bila jasho. Baada ya mawazo hayo, siku chache zilizopita nikaamua kwenda kwa mganga mmoja wilayani Bagamoyo ambaye alisifika sana kwa kutengeneza utaalamu huo. Nilifika kwa mganga, nikavua viatu kisha nikaingia ndani. Kama kawaida mganga alinikaribisha kwa mapambio ya ‘kilozi’. Zilipigwa chafya nyingi zilizosindikiza maneno yasioeleweka. Kabla sijamweleza shida iliyonipeleka pale, mganga akaanza kubashiri: “Kijana una matatizo makubwa, mambo yako hayaendi kuna watu wanakuchezea… umekuja kumtambua anayekufanya ushindwe kupiga hatua… “ Mganga mtaalamu mlozi aliendelea kuongea mambo mengi ambayo sikuhusiana nayo, nilipoo...