Posts

Nondo Zote za Kukusaidia Ufaulu Mitihani Usaili Walimu Masomo Yote

Image
Nimefanya tafiti kwa kipindi kirefu tangu ajira za ualimu zianze kupatikana kwa usaili. Katika tafiti hizo, nimegundua mengi ambayo nitakuleza ili nawe uweze kutumia ushauri wangu na uweze kufaulu mitihani hii, uwe selected! Vijana wengi wanaoomba ajira sasa wanaelekea kuamini mfumo hauko sawa, wanahisi kuna mchezo wanachezewa! Wanahisi pengine alama zile siyo zao na huenda matokeo yale yanatungwa sehemu. Sikuliacha hivihivi jambo hili, niliamua kuingia katika utafiti mimi mwenyewe, kwa kuwa kigezo ni vyeti na umri na wala hawajali sasa unafanya kazi wapi nilijisajili, nikachaguliwa kufanya masomo mawili, mtihani wa kwanza nilipangwa kufanyia chuo cha Kampala International, na mtihani wa pili nilipangwa kufanyia NIT. Kwa kuwa nilikuwa katika utafiti, nilijibu maswali yale tu ambayo nina uhakika wa asilimia 100 kuwa yalikuwa sahihi, maswali ambayo yalikuwa na utata sikuyajaza. Nilipotoka kwenye mtihani nilitambua kabisa kwamba lazima nipate alama fulani, matokeo yalipotoka, ilikuja ala...

Maswali 100 Kujiandaa na Mtihani Usaili Walimu Masomo Yote

Image
Kama unaelekea kufanya mtihani wa English au Geography, maswali haya usikubali kuyakosa, na kamwe usiingie katika mtihani wako, bila kuyasoma. Nafahamu unajiuliza kwamba, Geography na  English iweje maswali yafanane? Kama umechelewa kujua, mambo yamebadilika japo kwa kushtukiza, maswali sasa yanaangazia hesabu nyepesi, kompyuta, akili mnemba na taaluma ya ualimu! Lakini kabla sijajikita katika maswali, naomba nisimulie mkasa ili kukuondoa hofu ya kuwa ‘not selected’ badala yake uamini jambo moja tu, ‘selected’! Niweke wazi kuwa, nina mahusiano na mwanamke anayefanya kazi Sekretariati ya Ajira . Hata hivyo, kitengo chake wala hakihusiki na mitihani ya usaili walimu. Ninafichua kuwa, mahusiano yangu na yeye yamelegea, tukigombana akinitaka niache hiki ninachokifanya asije akafikiriwa vibaya nikamharibia ugali wake! Siwezi kuacha, ninafanya jambo hili kwa sababu mimi ni mwalimu, sipendi kuona walimu wanateseka kusoma mambo ambayo hayatoki. Kazi yangu ni kuwaambia linatoka jambo hili,...

Maswali 100 ya Kujiandaa na Usaili Walimu Somo la Kiswahili

Image
Katika mitihani ya usaili walimu , maswali haya ni msaada mkubwa. Kwa kuwa muda wa kusoma kila kitu hautoshi, maswali haya hutumika kama njia nzuri zaidi inayomfanya mwalimu apate kila kitu kwa muda mfupi na kumsaidia awe ‘selected’ kwenda ‘oral interview’ katika mitihani hii yenye ushindani mwingi. 1.  Katika kompyuta, ukibonyeza alama ctr+A unapata nini? A. Unafuta maandishi yote yaliyochaguliwa. B. Unachagua (highlight) maandishi au mafaili yote. C. Unahifadhi (save) kazi uliyokuwa unafanya. D. Unafungua faili jipya la kazi. Jibu: B 2.  Juma amewasha kompyuta yake, lakini anagundua kwamba, kila akicheza mziki, sauti haisikiki, afanye nini kama suluhisho? A.  Kununua spika mpya za kisasa zaidi. B. Kufuta nyimbo zote na kuziweka upya. C. Kukagua kama sauti imewekwa "Mute" au kama kadi ya sauti ina hitilafu. D. Kuzima kompyuta na kutofanya kazi yoyote. Jibu: C 3.  Program ya akili mnemba inayohusika na utengenezaji wa picha inayomilikiwa na kampuni ya google inaitwaj...

Maswali 100 Usaili Ajira za Walimu | Measurement and Evaluation

Image
Katika mitihani ya usaili ajira za walimu, changamoto kubwa katika usomaji ni mwalimu asome wapi, kwa sababu vitu vya kusoma ni vingi na havitoki vyote. Mwendelezo wa makala hizi unaeleza maeneo muhimu ambayo mwalimu anaweza akasoma na hivyo akaokoa muda huku akiwa na nafasi nzuri ya kufaulu. maeneo muhimu ya kusoma yanayotoka sana kwenye mitihani ya usaili walimu ni: CT 100 Introduction to Teaching , Education Psychology hususani Wanasaikolojia 10 , pamoja na measurement and Evalution. Makala hii inakuja na maswali 100 ya measurement and evalution, maswali haya hayajaacha kitu, ukiweza kujibu maswali haya, ukayafanyia mazoezi ya kutosha, tunakuahidi kwamba, hutakutana na swali jipya katika ukanda huu wa measurement and evaluation. Lengo letu ni kuhakikisha walimu wanasoma yale tu yanayotoka katika mitihani yao hivyo kuokoa muda na kuwasaidi kufaulu. Part 1 Section 1: Basic Concepts of Measurement & Evaluation 1.  Which process refers to translating learning experiences into nu...