Nondo Zote za Kukusaidia Ufaulu Mitihani Usaili Walimu Masomo Yote
Nimefanya tafiti kwa kipindi kirefu tangu ajira za ualimu zianze kupatikana kwa usaili. Katika tafiti hizo, nimegundua mengi ambayo nitakuleza ili nawe uweze kutumia ushauri wangu na uweze kufaulu mitihani hii, uwe selected! Vijana wengi wanaoomba ajira sasa wanaelekea kuamini mfumo hauko sawa, wanahisi kuna mchezo wanachezewa! Wanahisi pengine alama zile siyo zao na huenda matokeo yale yanatungwa sehemu. Sikuliacha hivihivi jambo hili, niliamua kuingia katika utafiti mimi mwenyewe, kwa kuwa kigezo ni vyeti na umri na wala hawajali sasa unafanya kazi wapi nilijisajili, nikachaguliwa kufanya masomo mawili, mtihani wa kwanza nilipangwa kufanyia chuo cha Kampala International, na mtihani wa pili nilipangwa kufanyia NIT. Kwa kuwa nilikuwa katika utafiti, nilijibu maswali yale tu ambayo nina uhakika wa asilimia 100 kuwa yalikuwa sahihi, maswali ambayo yalikuwa na utata sikuyajaza. Nilipotoka kwenye mtihani nilitambua kabisa kwamba lazima nipate alama fulani, matokeo yalipotoka, ilikuja ala...