Mfalme Anataka Kuniua | Sehemu ya Tano

Aliweza kuwatambua watu hao. Mmoja aliitwa Sasi, kosa lake Wizi. Wala hakusingiziwa. Sasi alikuwa mwizi aliyechukiwa na watu wote. Wa pili alikuwa Athu, yeye alifungwa kwa kosa la uharifu kama Sasi. Naye hakusingiziwa, alikuwa mwizi wa mifugo aliyechukiwa na wafugaji wote. Wa tatu aliitwa Sipe, alifungwa kwa hofu ya mfalme. Mfalme alimuogopa Sipe kuwa ipo siku angempindua. Sipe alikuwa mtu mwenye maneno ya busara. Mara chache alitabiri mambo yakatokea, hii ilimpa hofu mfalme kwa kuona Sipe atapendwa na watu kuliko yeye na kuleta mapinduzi. Sipe alionewa! “Hamjambo ndugu zangu?” Alisalimia Mako. “Hatujambo,” walijibu. Sipe akaendelea, “Hakuna aliyesalama, hata wewe Mako umeletwa humu? Umefanya kosa gani hasa?” “Ni uonevu tu,” alijibu Mako, akikaa katika kitanda cha majani, “nina mvua mbili za kunifanya niendelee kuwa hai. Nimehukumiwa kunyongwa kwa kosa la kuonekana katika ndoto ya malkia. Malkia kaota kwa sauti akisema ananipenda na hawezi kuniacha milele!” Wote walicheka, l