Posts

Showing posts with the label makala

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Image
Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 10,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. CV au wasifu ni kitu cha lazima kwa yeyote anayeomba kazi. Watu wengi wanaokosa kazi, tatizo huwa siyo wao, bali tatizo huwa ni CV zao. Kumekuwa na makosa mengi katika uandishi wa CV jambo ambalo limesababisha watafuta kazi wengi kushindwa kuitwa kwenye usaili. Makala hii itakueleza namna sahihi ya kuandika CV, utaitwa katika ‘interview’ nyingi endapo utaandika CV sahihi. Tena nakukumbusha, kila taaluma ina aina yake ya CV, CV ya rubani haifanani na CV ya injinia. Vivyo hivyo, CV ya mpishi haifananani na CV ya Mwalimu. Pia nakukumbusha usome jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi , kwani CV huenda pamoja na barua ya maombi ya kazi. Hatua ya kwanza nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiswahili na hatua ya pili nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiingereza halafu utachagua mwenyewe utumie lugha gani katika ku

Masomo Yaliyofundishwa Mtandaoni na Taasisi ya Elimu 12/05

Image
Mathematics-The Number System Quadrilateral  ENGLISH LISTENING SKILLS PROBLEM SOLVING PART A Masomo mapya yanawekwa katika ukurasa huu kila siku. Kuona masomo yaliyopita, mengi zaidi, ingia katika channel ya Taasisi ya Elimu huko YouTube. Kufuatia shule kufungwa nchini kwa sababu ya ugonjwa wa Korona, Taasisi ya elimu imeamua kutoa masomo kwa njia ya mtandao ili kuweza kuwasaidia wanafunzi wote nchini Tanzania. Nchini Tanzania , madarasa yanayotegemea kufanya mtihani mwaka huu ni: darasa la nne, darasa la saba, kidato cha pili, kidato cha nne na kidato cha sita. Hata hivyo, masomo hayatolewi kwa vidato vinavyofanya mtihani pekee, bali yanatolewa kwa vidato vyote. Masomo yanatolewa kwa kutumia televisheni na mtandao. Bila shaka mpango huu utawafaa sana wanafunzi ambao wako nyumbani kufuatia kufungwa kwa shule. Wanafunzi wawapo nyumbani, wazingatie ushauri wangu huu: Kwanza, wajilinde na ugonjwa wa korona kwa kufuata ushauri wa wataalamu ikiwemo: kunawa kwa maji tiririk

Jinsi ya Kufahamu Kiingereza cha Kujibia Mitihani

Image
Changamoto kubwa inayowakumba wanafunzi ni kumudu lugha ya kiingereza. Wapo wanafunzi ambao wanayaelewa vizuri masomo yao lakini tatizo linakuja katika kueleza majibu yao ambapo masomo yote isipokuwa Kiswahili hutumia lugha ya kiingereza. Kushindwa kumudu lugha ya kiingereza kunachangiwa na matumizi finyu ya lugha hii nchini. Watanzania wengi hutumia lugha ya Kiswahili katika shughuli zao za kila siku, hivyo wanafunzi wamekosa nafasi ya kufanya mazoezi ya kuzungumza lugha hii. Kama wewe ni miongoni mwa wanafunzi ambao wanashindwa kujibu mitihani na kupata matokeo mabaya kwa sababu ya kushindwa kuimudu lugha ya kiingereza, fanya mambo haya:      1.    Sikiliza lugha ya kiingereza Sikiliza mtu yeyote anayeongea lugha ya kiingereza hata kama huelewi. Sikiliza taarifa ya habari, watu wakizungumza katika televisheni na mwalimu akifundisha darasani.      2.    Zungumza lugha ya kiingereza Kiingereza kwa Watanzania wengi huambatana na aibu. Kama una aibu kuzungumza lugha ya ki

Matumizi ya Kiambishi ‘kwa’ | Matumizi ya Mofimu

Image
Kiambishi ‘kwa’ kina matumizi mengi, yafuatayo ni baadhi tu ya matumizi hayo:      1.    Kuonesha umiliki wa mahali Tazama mifano: Shangazi amekwenda kwa mjomba. Musa amelala kwa baba. Simba amepeleka maji kwa sungura. Ongeza mifano Zaidi.      2.    Kueleza sababu Mifano: Umepigwa kwa kuiba kuku . Umehukumiwa jela miaka mitano kwa kutukana watu. Amekufa kwa kujinyonga. Jaribu kuweka mifano yako mingine.      3.    Kuonesha sehemu ya kitu kizima Mifano: Amepata tano kwa mia moja. Musa ana akili sana, katika mtihani amepata sabini na tano kwa mia. Yahaya ana jitahidi, amepata saba kwa tisa. Endapo umeelewa dhima hii, weka mifano zaidi.      4.    Kuonesha muda uliochukuliwa na tendo fulani Mifano: Tulimsubiri kwa saa tisa. Walishauriana kwa saa saba. Walikesha kwa siku mbili wakila nyama na kucheza mziki. Ongeza mifano mitatu zaidi.      5.    Kulinganisha Mifano: Timu ya taifa ilishinda mbili kwa moja. Simba ilifungwa tano kwa nne.

Mchango wa Tipu, Bloomfield, Krapf Katika Kueneza Kiswahili

Image
Swali lote linasema, “Onesha mchango wa watu wafuatao katika kukuza na kueneza kiswahili nchini: Tippu Tipu, D.k Ludwig krapf, Broomfield na Askofu Edward steer.” Watu wengi wamesaidia katika kukua na kuenea kwa Kiswahili nchini Tanzania. Leo tutajadili mchango wa TippuTipu , Krapf, Broomfield na Askofu Edward Steer. Mchango wa Tippu Tipu katika kueneza Kiswahili Jina halisi la bwana huyu ni Hamad bin Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjeb. Alikuwa mwarabu mfanyabiashara wa watumwa. Tippu Tipu alisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili kwa sababu, alitumia Kiswahili katika biashara zake. Hivyo, kote alikopita, alieneza lugha ya Kiswahili na ikafahamika kwa watu wengi Zaidi. Mchango wa D.k Ludwig Krapf katika kueneza Kiswahili Krapf alisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili kwa sababu alitunga kamusi ya kwanza ya lugha ya Kiswahili. Kamusi hii ilisaidia kuuweka msamiati wa lugha ya Kiswahili katika kitabu kimoja. Mchango wa Broomfield katika kueneza   Kiswahili Mtaalamu

Jinsi ya Kuzuia Kusinzia Darasani Mwalimu Anapofundisha

Image
Kabla mwalimu hajaingia darasani, unakuwa na nguvu za kutosha na unazungumza na wanafunzi wenzako. Mwalimu anapoingia, hali inabadilika, kadri anavyoongea na wewe ndiyo usingizi unazidi kukolea. Badala ya kuelewa kipindi, unaishia kusinzia. Sasa mwalimu katoka na usingizi nao haupo. Ni kama umerogwa eeeh? Hapana, hujarogwa hilo ni tatizo la kawaida na karibia kila mwanafunzi hukutana nalo. Tatizo la kusinzia darasani. Kusinzia darasani kunaweza kukufanya uyachukie masomo na mwisho wake upate matokeo mabaya ya darasani kwani kile ulichotakiwa kukielewa hutakielewa kwa sababu ya kukosa usikivu. Tatizo hili linahitaji tiba , na zifuatazo ni njia za kufanya ili kuzuia kusinzia darasani.      1.    Pangilia vizuri muda wako wa kulala Lala muda unaofanana na amka muda unaofanana kila siku hata katika siku za mwisho wa wiki. Kwa mfano, kama unalala saa sita usiku na kuamka saa moja asubuhi, fanya hivyo siku zote. Muda wa kulala ni saa nane, hata hivyo kama ratiba yako ni ngumu, bado n

Mada za History Zinazotoka Zaidi Katika Mtihani Kidato cha 4

Image
Nimekuwa nikiulizwa swali hili na wanafunzi wangu wengi. “Mwalimu ni mada gani zinapenda kutoka katika mtihani wa History kidato cha nne?” wanaouliza swali hili wamegawanyika katika makundi matatu: Kundi la kwanza ni wanafunzi wavivu, wanataka wajue mada zinazotoka katika mtihani ili wasome hizo tu na wasihangaike kusoma mada zingine. Kundi la pili ni wanafunzi wanaotaka kufahamu waweke msisitizo wa kusoma mada gani zaidi. Na kundi la mwisho, huuliza bila kuwa na sababu maalumu, wao huuliza tu. Nasisitiza kuwa, siyo kosa kutaka kufahamu mada zinazotoka zaidi katika mtihani wa History kidato cha nne. Ni mada gani hutoka zaidi katika mtihani wa History kidato cha nne? Mada zote hutoka katika mtihani wa kidato cha nne. Ili uweze kufaulu mtihani wako wa History, unashauriwa usome mada zote za kidato cha kwanza, pili, tatu na nne, utaweza kufaulu vizuri mtihani wako. Pia, lengo la somo la History siyo kufanya mtihani pekee, lengo kuu ni kukupa maarifa ya Historia yak

Ni Somo Gani Kubwa Maisha Yamekufundisha?

Image
Nilikuwa katika kiota cha burudani, humo nilikwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa rafiki yangu mmoja ambaye tumefahamiana kwa miaka dahari. Katika meza niliyokaa, tulikaa wawili, mimi na dada mmoja ambaye hatukuwahi kuonana kabla. Hata hivyo, haikuchukua muda kufahamiana na kuanzisha mazungumzo. Wakati sherehe ikiendelea, dada aliniuliza swali, “Mwalimu Makoba, ni somo gani kubwa maisha yamekufundisha?” Nilitafakari kidogo, kisha nikajibu: “Nimejifunza kwamba hakuna njia ya mkato katika maisha. Watu wenye miili mizuri isiyo na vitambi wala unene kupitiliza wanastahili. Siyo uchawi .  Wamefanikiwa kwa maamuzi waliyofanya ikiwemo kupangilia mlo na kufanya mazoezi. Watu wenye mafanikio wanastahili. Mafanikio hayaji kwa bahati tena hayatokei kwa usiku mmoja. Wamefanikiwa kwa sababu waliamua kufanikiwa.” Nilimaliza kuzungumza, nikabaki kusikiliza mziki na kusukuma mafunda kadhaa ya kinywaji nilichopewa. Nilimsikia dada akirudia maneno niliyosema, “HAKUNA NJIA YA