Posts

Showing posts with the label kiswahiliformtwo

Utungaji wa Kazi za Fasihi Simulizi | Kiswahili Kidato cha 2

Image
Kazi za fasihi simulizi hazikutokea tu, kuna mtu alitunga kazi hizo. Mada hii, inaangazia utungaji wa kazi za fasihi simulizi: Utungaji wa mashairi Kanuni za Utungaji wa Mashairi Utungaji wa mashairi una kanuni mbili: 1. Fani 2. Maudhui Katika fani , mshairi azingatie lugha anayotumia kama: tamathali za semi, methali nahau na misemo pamoja na picha na taswira. Pia, mshairi azingatie kama mtindo wa shairi, kama ni shairi la kimapokeo au shairi la kisasa. Pia, mshairi azingatie muundo wa shairi lake, kama atatumia mistari miwili, mmoja, sita ama apendavyo yeye. Katika maudhui, unapotunga shairi zingatia wazo lako.   Mfano: ni lipi lengo la wewe kutunga shairi? Inawezekana unatunga shairi ili kuzungumzia hali ya umasikini unaoikumba nchi yako, au pengine una lengo tofauti. Pia, zingatia ujumbe au mafunzo yanayopatikana katika shairi ulilotunga. Unalenga kufikisha ujumbe gani? Mfano wa shairi lililotungwa kwa kuzingatia kanuni Kubaka Nimekuwa nikipima, najiuliza k

Uhifadhi wa Kazi za Fasihi Simulizi | Kidato cha Pili

Image
Uhifadhi wa kazi za fasihi simulizi ni kitendo cha kutunza kazi za fasihi simulizi ili zidumu kwa muda mrefu na ziweze kutumiwa na vizazi vingi zaidi. Njia za kuhifadhi kazi za fasihi simulizi Kichwani Hii ndio njia ambayo imekuwa ikitumiwa kuhifadhi kazi za fasihi tangu kale na inaendelea kutumika hadi leo. Kwa kutumia njia hii kazi ya msanii hukaa kwenye ubongo wa msanii, naye huweza kuiwasilisha kazi hiyo, wakati wowote bila gharama yoyote. Ubora wake 1. Uwasilishaji unafanyika wakati wowote Uwasilishaji wa kazi hiyo unaweza kufanyika wakati wowote bila kuhitaji kufanyika maandalizi yoyote, hususani ya kiufundi. 2. Hakuna gharama Msanii hahitaji kugharimia kitu chochote ili aweze kuitoa kazi ya fasihi kichwani, ni uamzi wake tu, anaweza kuimba papo kwa papo. 3. Kazi ya fasihi iliyohifadhiwa kichwani ni hai Hii ni kwa sababu msanii anakuwa ana kwa ana na hadhira yake. Kutokana na matumizi ya mbinu tofauti za kisanaa kama vile kucheza, kubadili sauti, miondoko na men

Uhakiki wa Kazi za Fasihi Simulizi | Kidato cha Pili

Image
Uhakiki wa kazi za fasihi simulizi huzingatia fani na maudhui ili kuchambua yale yaliyokusudiwa. Uhakiki wa ushairi Mashairi kama kazi nyingine za kifasihi huhakikiwa kwa kutumia vigezo sawa na vinavyotumika katika kazi nyingine za kifasihi. Vigezo hivyo ni kwa kuzingatia vipengele vyake viwili yaani fani na maudhui. Vipengele vya Fani na Maudhui katika Kuhakiki Ushairi Vipengele vya fani Uhakiki wa fani za ushairi ni uchambuzi wa kina na kuziweka wazi mbinu za kisanaa alizotumia mshairi katika kutunga kazi yake. Vipengele muhimu vya kuhakiki katika fani ya ushairi ni kama vifuatavyo: 1. Mtindo Jambo la kuonyesha hapa ni kwamba iwapo shairi ni la kimapokeo ama ni la kisasa. 2. Muundo Katika kuhakiki muundo wa shairi mhakiki inatakiwa aweke wazi mambo yafutayo: Idadi ya beti Idadi ya mistari na aina ya vibwagizo Idadi ya vipande Idadi ya mizani Aina na mpangilio wa vina 3. Wahusika Ikiwa shairi limehusisha wahusika ni vema pia mhakiki awabainishe 4. M

Matumizi ya Lugha Katika Miktadha Mbalimbali

Image
Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Rejesta Rejesta ni matumizi ya lugha kulingana na muktadha fulani. Katika mazingira ya kanisani, kuna mtindo wa lugha ambao ni tofauti na lugha ya kijiweni. Aina za rejesta Kuna aina nyingi za rejesta kwa madhumuni ya kukidhi haja ya mawasiliano katika mazingira ,masomo na taaluma mbalimballi.Kila mazinira yana aina tofauti ya rejesta mfano rejesta ya shuleni, rejesta ya hotelini, rejesta za mitaani, rejesta za mahakamani, rejesta za sokoni na nyingine nyingi. 1. Rejesta za Mitaani Haya ni mazungumzo yanayozungumzwa vijiweni nayo hueleweka na wazungumzaji wenyewe. Ni lugha ambayo huchipuka kutokana na kikundi cha watu ambacho ni kidogo. Mfano wa maneno yanayotumika sana mitaani ni kama vile “Mshikaji” (rafiki), Demu” (mwanamke)n.k. Kwa ujumla lugha ya mitaani ni lugha isiyo sanifu, ni lugha iliyojaa maneno ya mitaani ambayo yana